Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollha Ali Khamenei, ametetea makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 na kutumia lugha kali kumkosoa rais wa Marekani Donald Trump kwa kudanganya.

Kwa habari motomoto,
Movie mpyaaa!!
au Comedy za kufa mtu!!
Tafadhali comment kisha weka namba yako
TANGAZO




 
"Sitaki kutupa muda wangu kujibu kuropokwa na kelele za Trump," Ayatollah Ali Khamenei alisema
Bw. Trump amekataa kuthibitisha kwa bunge la Marekani kuwa Iran imetekeleza yaliyo kwenye mkataba huo.

Amatishia kufuta makubaliano yote ya rais Obama .

Trump alitaka mkataba huo kufanyiwa marekebisho kuizuia Iran kuunda silaha za nyuklia au makombora ya masafa marefu.

Ayatollah Khamenei alisema anakaribisha uungwaji mkono wa mkataba huo kutoka nchi za Ulaya, lakini akaongeza kuwa ikiwa Marekani itavunja makubaliano hayo Iran itayatupilia mbali.

Rais Trump pia aliilaumu Iran kwa kuzua misikusuko nchini Syria, Yemen na Iraq na kukiwekea vikwazo kikosi chenye nguvu nyingi Iran cha Islamic Revolution Guards Corps.

Sasa bunge la Congress litaamua ikiwa litaiwekea tena vikwazo vya kiuchumi, ambavyo viliondolewa kama sehemu ya makubaliano hayo.

Ikiwa hilo litafanyika Marekani itakuwa imekiuka makubaliano kwenye mkataba huo.

TANGAZO


Emoticon Emoticon

Copyright © 2017 Best Kesha Tv - Thank . You For . Visting .